Kujitoa kwa Mama Maria

Maria, Bikira mwenye enzi na mama mwenye huruma,
Malkia wa Mbingu na kimbilio la wakosefu,
sisi tunajiweka wakfu kwa Moyo wako Safi.
Tunajiweka wakfu kwako nafsi zetu kabisa na maisha yetu yote;
kila tulichonacho, kila tunachopenda, na kila ambacho ni sisi.
kwako tunatoa miili yetu, mioyo yetu na roho zetu;
kwako tunatoa nyumba zetu, familia zetu na nchi yetu.
Tunatamani kuwa kila kilicho ndani yetu na kinachotuzunguka kuwa chako,
na kishiriki faida za baraka yako ya kimama.
Na kuwa tendo hili la kujiweka wakfu kwako liwe bora na la kudumu,
tunarudia leo miguuni pako ahadi zetu
za ubatizo na Komunio Takatifu ya kwanza.
Tunaahidi kukiri kwa ujasiri na wakati wote
ukweli wa Imani yetu takatifu,
na kuishi kama wanavyostahiki Wakatoliki ambao ni watiifu
kwa maagizo yote ya Papa na Maaskofu katika ushirika naye.
Tunaahidi kufuata amri za Mungu na Kanisa lake,
hasa kuishika kitakatifu siku ya Bwana.
Pia tunaahidi kufanya matendo ya dini ya Kikristu,
na juu ya yote, Komunio Takatifu,
sehemu muhimu ya maisha yetu,
kwa kadiri tuwezavyo kufanya hivyo.
Mwisho, tunakuahidi,
Ee mtukufu Mama wa Mungu na Mama wa watu mwenye upendo,
kujitolea kwa moyo wote kwa huduma ya ibada yako takatifu,
ili kuharakisha na kuhakikisha,
kupitia utawala mkuu wa Moyo wako Safi,
kuja kwa Ufalme wa Moyo Mtakatifu wa Mwanao mpendwa,
katika mioyo yetu na mioyo ya watu wote,
katika nchi yetu na ulimwenguni pote,
kama mbinguni, pia duniani.
Amina.